Nuru ya Kiswahili https://nuru.udom.ac.tz/index.php/journal1 <p><em>Nuru ya Kiswahili</em> is an international peer-reviewed journal that aims to publish theoretical and empirical studies that contribute to our understanding of Swahili language, linguistics and literature. We accept manuscripts written in both Swahili and English languages.</p> The University of Dodoma en-US Nuru ya Kiswahili 2714-1969 Matumizi ya Fantasia katika Usanaji wa Filamu za Kiswahili Nchini Tanzania https://nuru.udom.ac.tz/index.php/journal1/article/view/46 <p>Makala hii inahusu matumizi ya fantasia katika usanaji wa filamu za Kiswahili nchini Tanzania. Fantasia ni miongoni mwa vipengele vinavyohusishwa na uhalisiajabu ambavyo hutumiwa na watunzi kusana kazi zao. Utafiti uliozaa makala hii ulitumia mbinu za kitaamuli. Data zilikusanywa kwa kutumia mbinu za uchambuzi matini na mahojiano. Filamu teule zilipatikana kwa kutumia mbinu ya usampulishaji lengwa. Uchambuzi wa data za makala umefanyika kwa kutumia Nadharia ya Fantasia. Filamu za Kiswahili za Kitanzania za <em>Jamila na Pete ya Ajabu</em> na <em>Nsyuka </em>zimetumika kama sampuli ya kubainisha mdhihiriko wa fantasia. Maeneo ambayo ufantasia umejitokeza katika filamu teule yamebainishwa. Maeneo hayo yamehusisha matukio ya kihadithi ya filamu pamoja na uwasilishaji wa ujumbe kupitia uigizaji. Aidha, ilibainika kuwa fantasia hutumika katika kuunda filamu kwa malengo ya ujengaji wa taharuki, ubunifu, na usisimuaji wa hisia ya mtazamaji. Vilevile, ilibainika kuwa matumizi ya fantasia katika filamu teule yana tija na madhara kwa usanaji na uwasilishaji wa filamu za Kiswahili kwa hadhira. Kufuatia matokeo haya, inapendekezwa watayarishaji wa filamu kuzingatia uwiano wa matumizi ya fantasia katika filamu ili kuepusha madhara yaliyoelezwa katika makala hii.</p> Gervas A. Kasiga Copyright (c) 2024 Nuru ya Kiswahili 2024-06-30 2024-06-30 3 1 1 26 Mbinu za Kukabiliana na Utamaushi katika Fasihi ya Kiswahili: Ulinganisho wa Wimbo Teule wa Jux na Diamond Platnumz na Kazi Teule za Kezilahabi https://nuru.udom.ac.tz/index.php/journal1/article/view/48 <p>Makala hii inakusudia kuonesha namna utamaushi unavyojitokeza katika wimbo wa “Enjoy” na kazi teule za Kezilahabi. Kutokana na maisha kuonekana kama kitu cha kukatisha tamaa (kutamausha) kwa kadri yalivyogubikwa na madhila mbalimbali, wimbo wa “Enjoy” unaonesha kuwa suluhisho ni kuamua “ku-<em>enjoy</em>” (kuyafurahia tu) kwa kadri mtu anavyoweza baada ya kupata nafasi ya kufanya hivyo. Hii ni tofauti na ilivyo katika kazi zingine za kidhanaishi, hususani kazi za Kezilahabi, ambazo zinaonesha kuwa suluhisho ni kujiua. Nadharia ya Udhanaishi iliongoza katika uchambuzi wa matini teule. Mbinu ya usampulishaji lengwa ilitumika katika kupata data zilizofanikisha makala hii. Data zilikusanywa kwa kutumia mbinu ya uchambuzi matini. Matokeo ya utafiti uliozaa makala hii yanaonesha kuwa maisha ayaishiyo mwanadamu ni mafupi, mwanadamu anao uhuru wake binafsi, kuna kukata tamaa kunakosababishwa na masuala ya mapenzi, dunia ni uwanja wa fujo—kila mtu amekuja kufanya fujo zake na mwisho atajiondokea, na, mwisho, masuala ya mahusiano ya kimapenzi ni huzuni tupu. Makala inahitimisha kwa kutoa mapendekezo kuwa suluhu ya kukata tamaa maishani siyo kujiua bali kuyafurahia maisha kwa kadri mtu awezavyo kwani kujiua hakutatui tatizo husika bali huweza kusababisha tatizo ama matatizo mengine. Aidha, iwapo mwanadamu ataamua kufanya fujo zake, ni vema afanye fujo za amani zisizowaathiri wengine. Uhuru binafsi uzingatie mipaka, kwani kila kitu kinapopitiliza huweza kuwa na madhara.</p> Alfred A. Malugu Caesar Jjingo Copyright (c) 2024 Nuru ya Kiswahili 2024-06-30 2024-06-30 3 1 27 42 Riwaya ya Rosa Mistika: Kurunzi ya Malezi ya Vijalunga https://nuru.udom.ac.tz/index.php/journal1/article/view/50 <p>Lengo la makala hii ni kujadili namna riwaya ya Kiswahili inavyosawiri suala la malezi katika familia, hususani malezi ya vijalunga. Makala inaangazia zila za changamoto za vijalunga pamoja na changamoto zenyewe; hatimaye, inapendekeza mikakati ya kuzidhibiti zila hizo. Utafiti na mjadala vimefanywa kwa kutumia Nadharia ya Uhalisia. Data zilikusanywa kwa kutumia njia za uchambuzi wa matini. Matokeo yanaonesha kuwa, kwa jumla, kiini cha matatizo ya vijalunga ni upogo wa malezi wanayoyapata katika familia au asasi za kielimu. Hali hii inasababisha vijalunga kunasa katika zila zinazowazunguka katika maisha yao. Matokeo hayo yamebainisha zila zifuatazo: mabadiliko ya mahitaji ya vijalunga, wazazi au walezi kukosa elimu ya kuishi na vijalunga, pamoja na kupwaya kwa mikakati ya umma kuhusu maisha ya vijalunga. Makala imebainisha kuwa zila hizo zinazaa changamoto zifuatazo: kukosa haki ya malezi, vijalunga kupata ujauzito wakiwa masomoni, kuambukizwa magonjwa, na kutengwa. Kutokana na zila na changamoto zilizobainishwa, mambo yafuatayo yanapendekezwa ili kujenga ustawi wa vijalunga. Mosi, wazazi na walezi wapatiwe elimu ya kuishi na vijalunga. Pili, utoaji wa elimu kuhusu mabadiliko ya mahitaji ya vijalunga uimarishwe. Tatu, mikakati ya umma kuhusu maisha ya vijalunga iimarishwe. Hatimaye, kupitia hoja hizo, tumedhihirisha kuwa riwaya ya <em>Rosa Mistika</em> inafaa kuwa kurunzi ya malezi ya vijalunga ikiwa itasomwa au kufundishwa kwa umakini.</p> Athumani A. Ponera Copyright (c) 2024 Nuru ya Kiswahili 2024-06-30 2024-06-30 3 1 43 69 Assessment of Kiswahili Poetry Teaching and Learning in Rwanda: A Contextual Perspective https://nuru.udom.ac.tz/index.php/journal1/article/view/51 <p>While Kiswahili poetry has been reported to be an intriguing genre, students claim to face challenges when studying it. This paper aims to assess the teaching and learning processes of Kiswahili poetry in Rwanda, focusing on its relevance to the social and cultural context. The paper has examined six crucial aspects of teaching and learning to achieve its objectives: comprehending poetry and its importance, the Kiswahili subject syllabus, the subject content, learning objectives, the actual process of teaching and learning, and the evaluation of teaching and learning. The study is grounded in the Contextual Learning Theory. The study, purposively, selected 6 secondary school teachers of Kiswahili who teach in language combinations and their corresponding students in Gasabo District. The findings indicate that the problem of context has not been, thoroughly, considered in the teaching and learning of Kiswahili poetry in Rwanda despite its clear impact on the process. Consequently, students face difficulties in fully grasping this crucial subject matter. Hence, the study proposes solutions on better integration of the teaching of Kiswahili poetry with the Rwandan context and, further, recommends teachers to prioritize the contextual aspects of Rwanda when teaching Kiswahili poetry.</p> Vedaste Mudaheranwa Wallace K. Mlaga Copyright (c) 2024 Nuru ya Kiswahili 2024-06-30 2024-06-30 3 1 70 98